Habari
Shamim Mwasha na mume wake wapandishwa kizimbani kwa tuhuma za kukutwa na Dawa Za Kulevya
Mmiliki wa Blog ya 8020 Fashion, Shamim Mwasha na Mume wake, Abdul Nsebo maarufu Abdukandida wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo wakikabiliwa na tuhuma ya kukutwa na Dawa Za Kulevya aina ya heroin.
Wanandoa hao wanadaiwa kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroin zenye uzito wa zaidi ya Gramu 232 nyumbani kwao Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam na walikamatwa siku ya Mei Mosi, 2019