Burudani
Siri ya mahusiano kati ya Rihanna na Drake yaanza kufichuka
Rihanna na Drake wamekuwa kwenye mahusiano ya siri kwa mwezi mmoja sasa.
Hivi karibuni Rihanna alihusishwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Leonardo DiCaprio baada ya kuonekana wakiwa wote kwenye tamasha la Coachella.
Jarida la People limeripoti kutoka chanzo cha habari kuwa Rihanna na Drake wameamua kuweka mahusiano yao kuwa siri kwa wakati huu watu wasiyajue.
Miaka kadhaa nyuma Chris Brown aliwahi kugombana Drake kutokana na tuhuma za kutoka na Rihanna.