Habari
Taasisi ya Imam Bukhari yalia na watuhumiwa wa ugaidi kusota maabusu
Mwenyekiti wa taasisi ya Imam Bukhari, Sheikh khalifa Khamis ameeleza kwa masikitiko makubwa mambo ambayo amedai wanaendelea kufanyiwa watuhumiwa wa kesi mbalimbali za ugaidi hapa nchini hususani Mashekhi wa Uamsho waliokamatwa Visiwani Zanzibar. Amesema hayo leo wakati akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es salaam, ambapo alimtaka Rais Magufuli kuingilia sakata hilo.