Habari
Ubungo Plaza: Mahakama imetoa kibali cha kuifunga Blue Pearl Hotel (Video)
Mkurugenzi wa Jengo la Ubungo Plaza, Harun S. Mgude amefunguka kwa kuzungumzia sababu ya kumfukuza mpangaji wake ambaye alikuwa anamiliki Hotel ya Blue Pearl na kushikilia baadhi ya mali zinzomiliwa na hotel hiyo kupitia kampuni ya Udalali ya Yoyo kwa madai ya kushindwa kulipa kodi ya pango ya tsh bilioni 5.7. Bosi huyo amesema mpangaji wake huyo alikuwa ni mdaiwa sugu toka mwaka 2014 na wiki iliyopita walipewa amri na Mahakama ya kumfukuza katika jengo pamoja na kumtaka alipe deni hilo.