Burudani
Uchaguzi wamtia hofu Dayna kuachia ngoma mpya
Dayna Nyange amesema amewaandalia kazi nyingi mashabiki wake lakini anashindwa kuziachia kutokana vuguvugu la uchaguzi linaloendelea.
Akizungumza na Bongo5 leo, Dayna amesema ingawa uchaguzi umepita lakini bado masikio ya watanzania hayako sawa kupokea muziki mpya.
“Bado watanzania ndio wanatoka kwenye uchovu wa uchaguzi, nina nyimbo nyingi ila siwezi kutoa kwa sababu bado naona hali si shwari kwa watu ambao tunahitaji wasikilize muziki wetu. Kwa mimi binafsi nachukua nafasi hii kujiandaa zaidi ili nije kufanya mambo mazuri zaidi baada ya hali kutulia zaidi pamoja na rais kuapishwa,” amesema Dayna.