Michezo

USAJILI: Yanga yamnasa golikipa wa Serengeti Boys

Klabu ya Yanga yenye maskani yake mitaa ya Jangwani jijini Dar es salaam, imefanikiwa kunasa saini ya Golikipa wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Ramadhani Kabwili.

Yanga SC wametoa taarifa hizo kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii kuwa amesaini kwa kandarasi ya miaka mitano.

“Ramadhani Kabwili,golikipa wa timu ya Taifa ya Vijana ya Tanzania ?? (Serengeti Boys) amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka mitano”,imesomeka ripoti iliyotolewa na Yanga.

Klabu ya Yanga ni miongoni mwa klabu zilizosajili wachezaji wengi msimu hii ni kutokana na nguvu ya pesa walizopata baada ya udhamini wa Kampuni ya kubashiri ya SportPesa.

By Godfrey Mgallah

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents