Burudani

Utafiti: Tanzania yabainika kuwa nchi ya kwanza isiyo aminifu duniani!

Utafiti umebaini kuwa wananchi wanaoishi kwenye nchi zilizotawaliwa na rushwa nao pia hujikuta wakikosa sifa ya uaminifu.

09M_Honest Table

Utafiti huo umebainisha kuwa uaminifu binafsi huwa mkubwa kwenye jamii zenye matatizo machache ya rushwa, ukwepaji kodi na utapeli wa kisiasa.

Wakati ambapo Austria, Uholanzi na Uingereza zimeshika nafasi ya kwanza katika nchi aminifu duniani, Tanzania na Morocco ambazo ubora wa taasisi zake ulibainika kuwa wa chini, zilifanya vibaya.

Utafiti huo ulifanywa na chuo kikuu cha Nottingham na kuhusisha nchi 159.
Walitumia taarifa zilizopo kuanzia mwaka 2003 za utapeli kisiasa, ukwepaji kodi na rushwa.

Utafiti huo ulibaini kuwa watu wanaoshi kwenye nchi zenye matukio machache ya uvunjaji sheria, walikutwa na uwezekano mdogo wa kudanganya ili kupata fedha ukilinganisha na nchi zenye matatizo ya rushwa.

Ulidai kuwa uwepo wa matukio ya uvunjaji sheria, huwafanya watu kupindisha ukweli.

Chanzo: Daily Mail

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents