Hii ni video mpya ya Hemedy PHD ya wimbo wake ‘Imebaki Story’ iliyoongozwa na Kwetu Studios na kuhaririwa na Adam Juma.
https://youtu.be/m9p1Y6QHSDY
Video hii imefanyika kwenye mikoa minne.
“I am still proud kushoot bongo sababu locations kali tunazo,” Hemedy aliiambia Bongo5 hivi karibuni.
“Nahamasisha wasanii wenzangu kutumia more nyumbani na kupatangaza pia,” aliongeza.
Alisema video hiyo imefanyika kwenye mikoa ya Arusha, Morogoro, Dar es Salaam na Manyara na kwamba imemgharimu takriban shilingi milioni 15.
“Thank God niliweka malengo ya kufanya kitu kizuri home, nafikiri ni video yenye kiwango kizuri na inaitangaza Tanzania pia sababu nimetumia sehemu kubwa kuonyesha uzuri wa nchi.”