Habari

Wananchi wamtaka Rais wa Korea Kusini ajiuzulu

Maelfu ya wananchi wa Korea Kusini, waliandamana kwenye mji mkuu Seoul, Jumamosi, kumtaka Rais Park Geun-hye ajiuzulu.

2013-10-30-park-president

Polisi wamekadiria kuwwa karibu waandamanaji 12,000 walishiriki.

Rais wa Korea Kusini yupo kikaangoni kwa kudaiwa kuvujisha nyaraka za serikali kwa rafiki yake. Wananchi wanataka na mawaziri kadhaa nao wajiuzulu.

Jumanne iliyopita, Bi. Park alikiri kumuonesha rafiki yake Choi Soon-sil nyaraka hizo. Choi ambaye hana nafasi yoyote serikalini, alikuwa akimsaidia Park maoni kwenye hotuba zake kabla ya uchaguzi wa Rais mwaka 2012.

Rais huyo ameomba radhi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents