Burudani
Wasichana wengi wanamtamani mpenzi wangu – Linah
Linah anaamini kuwa wasichana wengi wanamtamani mpenzi wake, Williams Bugeme aka Boss Mutoto.
Linah ameiambia E-Newz ya EATV kuwa anachojali yeye ni kuona mambo yake na mpenzi wake huyo kwenda sawa.
“Kikubwa ni changamoto ambazo nakutana nazo, kwahiyo mimi namjali mwanaume wangu kwa sababu ana mwonekano mzuri na ni mwanaume kila mwanamke anatamani kuwa naye,” alisema.
“Kwahiyo kwangu mimi nachukulia kama changamoto na pia vilevile nakuwa proud kwa kuona mtu wangu mimi ni mtu poa. Siwezi kumpangia Mungu anachopanga, malengo ya kila mtu anataka kufika mbali na mpenzi wake,” aliongeza Linah.