Habari
Watu 9 wafariki kwa ajali Mbeya
Mbeya: Ripoti zinaeleza Watu tisa wamefariki dunia na wengine 23 kujeruhiwa baada ya gari aina ya Mitsubishi walilokuwa wakisafiria kutoka Mbeya kuelekea Mbarizi kupinduka baada ya kugongwa kwa nyuma na lori katika Mlima Iwambi Mkoani
Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amethibitisha ambapo amesema Lori lililokuwa linatoka Mbeya kuelekea Tunduma liligonga gari aina ya Mitsubishi kwa nyuma na kusababisha vifo vya Watu tisa (Wanaume watano na Wanawake wanne) a majeruhi 23 (Wanaume 13 a Wanawake 10)
“Majeruhi walikimbizwa Hospitali teule ya Mbarizi, wengine wameruhusiwa, mpaka sasa hivi majeruhi 20 wapo Hospitali”