Michezo
Wenger avunja rekodi ya Ferguson EPL
Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amevunja rekodi ya Ligi Kuu nchini Uingereza kwa kuzifunga timu nyingi zaidi kuliko makocha wote.
Wenger ambaye anamiaka 21 ndani ya kikosi cha The Gunners amezifunga timu 45 na kumzidi Sir Alex Ferguson ambaye amezifunga timu 44 pekee.
Matokeo ya ushindi wa mabao 2-0 waliyopata Arsenal hapo jana dhidi ya Brighton yanamfanya mfaransa huyo kufikia rekodi hiyo ambayo haijawai kufikiwa na kocha yoyote wa Ligi Kuu nchini Uingereza EPL.
Kocha Arsene Wenger wa Arsenal, amesema kama FC Barcelona watakuwa ‘siriaz’ na uamuzi wao wa kuhama La Liga na kucheza Premier League litakuwa jambo zuri lakini wataongeza ugumu kwa kiasi kikubwa.