50 Cent athibitisha kuachia hili mwaka huu
Unatamani kuiona albamu mpya ya 50 Cent mwaka huu? Basi kaa tayari kwa hilo.
Rapper huyo amethibitisha kuwa kabla ya mwaka huu haujafika mwisho ataachia albamu yake mpya. Cent amethibitisha hilo wakati alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Access Hollywood Live.
“I have an album that I’ve been waiting to put out. It’ll be [out at] the end of the year. It won’t be as smart as the JAY-Z record. I wanted to make music that people have fun to. You can get it immediately, without having to sit and analyze,” amesema 50.
Siku chache zilizopita 50 Cent aliiponda albamu mpya ya Jay Z ‘4:44’ kwa kusema albamu hiyo inafaa kusikilizwa kwenye mchezo wa golf kwa kuwa imekaa kiutu uzima sana na siyo kwa ajili ya watu kufurahia, je atakapoachia albamu yake itakuwaje?