Michezo
Aguero: Nitarudi Argentina mkataba wangu ukiisha Man City 2019
Mshambuliaji wa klabu ya Manchester City Sergio Aguero amesema kuwa atahama klabu hiyo wakati mkataba wake utakapokamilika Raiya huyo wa Argentina ana mkataba wa miaka mitano ambao utamalizika katika msimu wa 2018-19.
Amesha ifungia City mabao 128 tangu aliposajiliwa na klabu hiyo kutoka Atletico Madrid kwa kitita cha pauni milioni 38 mwaka 2011,na kushinda ubingwa wa ligi ya Uingereza mara mbili.
Aguero mwenye miaka 27 alikiambia kituo kimoja cha redio nchini Argentina kwamba ni wazi atarudi katika kilabu yake ya kwanza ya Independente na kustaafu.
”Hapa City wanajua ni nini ninacho taka kufanya,wanajua nataka kurudi Argentina”,aliongezea.