Burudani

Alikiba ashinda tuzo Ufaransa, awabwaga Davido, Sarkodie, Yemi Alade na wengine

Fresh kutoka kushinda tuzo ya video bora ya mwaka (Aje) kwenye tuzo za Soundcity MVP za Nigeria, Alikiba ameongeza nyingine wikiendi hii.

Mkali huyo ameshinda tuzo ya Chaguo la Watu (Prix du Public) kwenye tuzo za Ufaransa za Wana Music Awards zilizotolewa Ijumaa hii.

“Hii ilikuwa ni tuzo pekee ambayo ilikuwa wazi kwa watu kupiga kura mwaka huu na msisimko uliozalishwa na tuzo hii umevuka matarajio yetu kwa kuwa na majadiliano zaidi ya 30,000 kwenye matangazo yetu kupitia mitandao ya kijamii,” waandaji wa tuzo hizo Wana Corp wameandika kwenye tovuti yao.

“Mshindi, Alikiba wa Tanzania aliweza kujikusanyia jamii kubwa ya mashabiki, ‘mashabiki damu wa Alikiba’ kuweza kuuchukua ushindi. Mwaka huu umekuwa wa mafanikio kwa Alikiba akiwa na sahihi katika label kubwa ya Sony, kushinda tuzo ya kimataifa ya MTV Europe Music Awards kama ‘Best African Act’ na yote kwa yote kuwa na moja ya video bora za mwaka na Aje,” wameongeza.

“The main information of this “Public Prize” is to see that our small website created in France can have links with a country like Tanzania thanks to Alikiba. Just for that, we say thank you to all those fans who have mobilized: a new link between Paris and Dar-Es-Salaam has been formed,” wamesisitiza.

Kwenye tuzo hiyo Alikiba alikuwa akichuana na Davido, Eddy Kenzo, Sarkodie, Serge Beynaud, Yemi Alade. Kulikuwa na jumla ya vipengele 14. Kundi la Sauti Sol nalo limeshinda kipengele cha kundi bora la mwaka.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents