Atumia Nyoka kama barakoa kujikinga na Corona
Msafiri huyo aliyekuwa amevaa barakoa yake ya nyoka alikuwa amejizungushia katika shingo na mdomoni, alionekana katika basi lililokuwa linatokea Swinton kuelekea mji wa Manchester nchini Uingereza siku ya Jumatatu.
Abiria mmoja, alisema anadhani abiria huyo alikuwa amevaa barakoa ya kisasa tu mpaka alipomuona nyoka huyo akiteleza katika chuma cha kushikia mikono.
Mkuu wa usafirishaji wa Manchester amethibitisha kuwa alikuwa ni nyoka na sio barakoa halisi.
Aliongeza kusema kuwa nyoka huyo hakuwasumbua abiria wenzake.
Msemaji wa usafiri wa Manchester alisema: “Muongozo uliotolewa na serikali umesema wazi kabisa kuwa barakoa zinazoruhusiwa sio lazima zile za upasuaji bali abiria anaweza kutengeneza barakoa yake anayoridhika nayo na kuivaa akiwa huru.
“Ingawa kuna kiwango kidogo tu tafsiri kamba inaweza kumaanisha hili, hatuamini maagizo hayo yalifikia kiwango cha mpaka kuruhusu ngozi ya nyoka-hususan wakati imeambatana na nyoka .”