Michezo
B-Ball Kitaa Tournament kuanza Jumapili hii jijini Dar es Salaam
Mashindano ya mpira wa kikapu ya B-Ball Kitaa yanatarajiwa kuanza Jumapili hii kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Mashindano hayo yatahusisha timu nane ambapo mshindi ataibuka na kitita cha shilingi milioni 1.2. Kutakuwepo pia na zawadi zingine katika shindano la kudunk, kufunga point 3 na pia kutakuwepo na freestyles ambapo mshindi atazawadiwa shilingi laki 5.