Burudani
Barnaba apanga kuvunja Record Billcanas
Mwanamuziki kutoka nyumba ya Vipaji Tanzania ‘THT’ Elias Barnaba ‘Barnaba Boy’, amesema katika usinduzi wake wa wimbo wa Gubegube na gube dume, anatarajia kuanika maisha yake ya miaka mitano katika muziki.
Barnaba amesema katika uzinduzi huo atafanya vitu ambavyo hajawahi kufanya na yoyote, kwa kutapambwa na Red Capert na Blue Capert.
Aidha amesema pia atagawa Cd, Pen na watu watasaini Out graphi yake, na kuupiga wimbo huo kwa mara ya kwanza.
Itakuwa ni siku ya kipee, hakika kila mmoja atajua Barnaba anafanya nini kwenye muziki na lengo langu katika muziki huu, Uzinduzi utafanyika leo Billcanas, na ndiyo itakuwa mara yake ya kwanza kufanya nyesho katika club hiyo maarufu tangu alipoanza muziki.