Burudani
Binamu kuangusha track mpya soon
Mwana FA ambaye ni mkali wa mashairi katika fani ya muziki wa Bongo hivi karibuni anatarajia kutoa track mpya ambayo iko harakati za kuimalizia akiwa amemshirikisha msanii Belle9 kutoka pande za Morogoro.
Mwana FA aliiambia Bongo5 kuwa track hiyo anairekodia katika studio za MJ Records pande za Masaki chini ya producer makini Marco Chali.
Hata hivyo pamoja na kubanwa ataje jina la track hiyo…Mwana Fa hakuwa tayari kwa maelezo kuwa haukuwa muda muafaka…na kuahidi kufanya hivyo muda utakapojiri…huku akisisitiza kuwa track hiyo itasikika katika vituo vya radio mapema January 2011.