Michezo

Borussia Dortmund yaushangaza ulimwengu

Klabu ya Borussia Dortmund leo tarehe 10 Novemba 2017, imeushangaza ulimwengu wa soka baada ya kutangaza kumfukuza kazi kocha wake, Peter Bosz na kumuajili Peter Stöger.

Peter Bosz amepoteza michezo 12 tangu ajiunge na klabu hiyo na kitu pekee cha kushangaza ni kwamba Dortmund wamemuajili kocha ambaye ametimuliwa na klabu ya inayoshika mkia wa ligi kuu nchini Ujerumani Bundesliga.

Kuchaguliwa kwa Peter  Stöger kumezua gumzo kubwa nchini Ujerumani kwani wadau wengi wa soka wanasema Dortmund wamekosea kumsajili Kocha ambaye mwenye historia mbaya kwenye kufundisha timu za Ujerumani.

Peter Stoger amepoteza mechi 8 na kupata sare 3 kabla ya kutimuliwa na klabu ya FC Cologne ambayo inashika mkia kwenye msimamo wa Bundesliga. Ambapo imeelezwa kuwa ndio kocha wa kwanza kuanza vibaya kwenye tangu ligi hiyo ianzishwe.

Na hii inakuwa ni hatua ya kwanza kwenye historia ya Ligi kuu nchini Ujerumani kwa kocha mwenye karba hiyo kuajiliwa na klabu kubwa nchini humo.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents