Habari

Bunge la Lebanon laipa jeshi nguvu, laidhinisha hali ya dharura Beirut

Bunge la Lebanon leo limeidhinisha hali ya dharura katika mji mkuu Beirut katika kikao chake cha kwanza tangu mlipuko uliosababisha vifo na hasara kubwa wiki iliyopita.

Lebanese army soldiers are deployed during a protest in the aftermath of last week's deadly blast in Beirut [Thaier al-Sudani/Reuters]

Idhinisho hilo linalipa jeshi la nchi hiyo nguvu kubwa wakati ambapo ghadhabu miongoni mwa wananchi zinazidi na mustakabali wa kisiasa nchini humo ukiwa haubainiki.

Kabla kujiuzulu serikali ya Lebanon ilikuwa imetangaza hali hiyo ya dharura ingawa ilikuwa inahitaji kuidhinishwa na bunge.

Hatua hiyo imekosolewa na makundi ya kutetea haki za binadamu na wakosoaji wengine wanaosema serikali ya kiraia tayari ilikuwa inatumia nguvu dhidi ya waandamanaji kwa sababu ya janga la virusi vya corona.

Bunge la Lebanon linafanya vikao vyake katika eneo lengine mbali na bunge kwa ajili ya kuweka umbali wa mtu hadi mtu kutokana na virusi vya corona na pia raia wa nchi hiyo wamekusanyika nje ya bunge wakiandamana na kutaka wanasiasa wote waachie ngazi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents