Burudani
Cash Money wasaini mkataba na Apple Music
Rapper Birdman na lebo yake ya Cash Money wamesaini mkataba na kampuni ya music ya Apple.
Huu ni mkataba wa kwanza wa kampuni hiyo kusaini kusambaza kazi za lebo tofauti na ilivyozoeleka wamekuwa wakisambaza kazi za msanii mmoja mmoja pekee.
Hata hivyo mkataba huo hautawagusa Lil Wayne na Nicki Minaj kwa kuwa wao walishasaini mkataba muda mrefu na kampuni ya Tidal ya Jay Z.
Wasanii wengine wanaomilikiwa na kampuni hiyo ya Apple Music ni pamoja na Drake, Taylor Swift, DJ Khaled, Future na wengine wengi.