Michezo
CEO wa zamani wa Microsoft, Steve Ballmer ndio mmiliki mpya wa timu ya LA Clippers
Timu ya kikapu ya Los Angeles Clippers imepata mmiliki mpya.
Steve Ballmer (kushoto akiwa na kamishna wa NBA, Adam Silver mwezi May) ndiye mmiliki mpya rasmi wa Clippers
Mwenyekiti Mtendaji wa zamani wa kampuni ya Microsoft, Steve Ballmer ameshinda dau la kuinunua timu hiyo kutoka kwa Shelly Sterling, mke wa mmiliki wa zamani wa timu hiyo, Donald Sterling.
Ballmer, ameinunua timu hiyo kwa dola bilioni 2. Ameichukua timu hiyo baada ya wiki kadhaa za mvutano wa kisheria kati ya Shelly and Donald Sterling, bilionea mwenye miaka 80 ambaye mapema mwaka huu alipigwa marufuku kujihusisha na NBA kwa kuongea kauli za kibaguzi dhidi ya watu weusi.