Mwanamuziki alifunga kitandawili juu ya safari mpya ya kimuziki kwa kuhama bendi yake iliyomkuza Twanga Pepeta, Chaz Baba sasa ametangaza kwa kukifungua kitangawili hicho kwa kusema tayari ameshaini mkataba wa miaka miwili na bendi ya Mashujaa almaarufu kama bendi ya Mama Sakina.
Mwanamuziki huyo anasema baada ya mkataba wake kuisha kwa muda wa miaka miwili basi ataendelea kuangalia upepo unavuma upande upi, kwani anatarajia meneja wake ndiye atakuwa akimuelekeza kazi gani afanye baada ya mkataba.
Bendi hiyo inatarajia kumtambulisha leo katika viwanja vya Makumbusho, show itakayoanza saa mbili usiku, wakisindikizwa na Mapacha watatu, na Extra Bongo Wazee wa kujinafasi chini Ali Choki.