Habari

China yagundua teknolojia mpya itakayorahisisha usafiri

Wakati serikali ya Tanzania ikipambana kupunguza tatizo la usafiri na msongamano wa foleni kwa wananchi wake, Wachina wameanza kugundua teknolojia mpya ya usafiri ambayo itasaidia kupunguza foleni barabarani.

BASI

Teknolojia hiyo mpya ya usafiri haitaathiriwa na foleni za barabarani ambayo yatakuwa ni mabasi mapana ambayo kwa chini yanaruhusu magari kupita na kupishana bila wasiwasi wowote, huku yenyewe yakisafiri bila kulazimika kusimama kusubiri magari yapite, isipokuwa kwenye njia panda na kwenye taa za barabarani pekee.

Aidha basi hilo litakuwa na uwezo wa kubeba watu 1,200 kwa mara moja. Linatajwa kuwa ufumbuzi wa msongamano wa magari barabarani. Pia, lilifanyiwa majaribio kwa mara ya kwanza wiki iliyopita huku magari mengine madogo yenye urefu wa futi 6.6 yanapita chini ya gari hilo jambo ambalo linaelezwa hupunguza idadi ya magari kwenye msongamano. Basi hilo linalotumia umeme na inaelezwa kwamba, linaweza kusafiri kilomita 60 kwa saa moja.

Shenzhen Hashi ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya China TBS Limited iliyohusika kutengeneza magari hayo amesema wametumia kiasi cha dola 74.1 kutengeneza basi hilo moja ambalo utengenezaji wake ulianza tangu mwaka 2010.

Tazama video hapa

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents