Michezo
Christiano Ronaldo ampiku Shakira na kuwa staa mwenye wafuasi wengi zaidi Facebook duniani
Mchezaji wa Real Madrid ya Uhispania na Ureno, Christiano Ronaldo kwa sasa ndiye mtu maarufu zaidi duniani kwenye mtandao wa Facebook. Ronaldo mwenye umri wa miaka 30 amempiku mwanamuziki maarufu kwa kunengua kiuno, Shakira kwa kuwa na wafuasi zaidi ya milioni 107.
Ronaldo ana wafuasi 107,096,356 wakilinganishwa na 107,087,100 wa Shakira. Ronaldo aliweka rekodi kwa kuwa mchezaji maarufu zaidi duniani alipotimiza wafuasi milioni 100 mwezi Oktoba mwaka uliopita.