Burudani
Ciara na rapper Future wapata mtoto wa kiume, wampa jina la baba yake
Mwimbaji Ciara na mchumba wake rapper Future wamepata mtoto wa kiume waliyempa jina la Future Zahir.
Ciara na Future
Ciara (28) amejifungua siku ya Jumatatu asubuhi (May 19) huko Los Angeles, Marekani.
Future Zahir ni mtoto wa kwanza kwa Ciara na kwa Future anakuwa mtoto wanne.
Jana Ciara alipost picha ya mkono wa mwanaye Instagram na kuandika, ‘FUTURE ZAHIR WILBURN 9lbs 10oz May 19 2014’.