Michezo

Diafra Sakho kukosa michuano ya mataifa bingwa barani Afrika

Mchezaji wa klabu ya West Ham na timu ya taifa ya Senegal, Diafra Sakho hatacheza katika mechi ya kuwania kombe la mataifa bingwa barani Afrika baada ya kuripotiwa kuwa hatacheza kwa kipindi cha wiki nane zaidi kutokana na jeraha.

Klabu ya West Ham ilitoa taarifa tarehe 30 mwezi Novemba kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 hatacheza kwa wiki sita ikimaanisha kuwa hatarejea uwanjani hadi kati kati ya mwezi wa Januari.

Lakini koacha wa West Ham Slaven Bilic, amesema kuwa Sakho huenda asicheze kwa kipindi cha wiki nane na huenda sasa akarejea kati kati ya mwezi Februari.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents