Burudani

Dj Khaled kuanza na Davido kuiteka Afrika

Dj khaled kutokea nchini Marekani ana mipango ya kuutangaza zaidi muziki barani Afrika.

Dj huyo ambaye ameshafanya kazi na wasanii wakubwa Marekani amesema moja ya mipango yake ni kufanya kazi na wasanii wakubwa wa Afrika.

Hii ni baada ya kukutana na msanii wa Nigeria, Davido na kueleza hayo. Huenda Davido tayari yupo katika mipango ya Dj Khaled.

Dj Khaled ameweza kufanya kazi na wasanii wakubwa Marekani kama Rihanna, Bryson Tiller, Justin Bieber, Lil Wayne, Demi Lovat, Jay Z na Future.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents