Habari
Dkt Magufuli, Mwinyi kuapishwa tarehe hii (+Video)
Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amesema Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ataapishwa tarehe 5/11 / 2020 Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Dkt Abbas ameongeza kuwa kwa upande wa Zanzibar, Dkt Hussein Mwinyi ataapishwa siku ya Jumatatu ya tarehe 3/11/2020.