Dogo watatu wafanya balaa Maisha Club
Katika wikiend hii, ukumbi wa New Maisha Club ulijukuta ukivamiwa na wingi wa watu hadi kushindwa kwa kuchezea baada ya kuwadondosha wadogo wa tatu wenye staili tofauti kabisa katika uimbaji kwenye muziki huu wa Bongo fleva.
Hapa nazungumzia Dogo Janja, Young D na Aslay ambao walikuwa gumzo na kusukumana na kuvutana kwa michano pale jukwaani ili kila mmoja amwangushe mwenzake. wapo wengine wakajisahau na kuwaita wadogo wenzake wazee, ilimradi kuleta mbwembwe. Ukumbini hapo watu walijaa kuliko kawaida, hadi mtu kutiririka jasho hata kama ulikuwa umekaa tu….
Dogo Aslay alikuwa wa kwanza kupanda na kitu chake, ‘Naenda kusema’ kwakuwa alikuwa na show nyingine ndani ya Billcanas usiku huo huo katika uzinduzi wa video ya Chege na Temba ‘Kama ni Genstle au Sharobaro.
Dogo Janja alifuata baadaye akaja kupigwa jeki na mtu mzima Tunda man kutoka makao makuu Tip Top
Young D, Young Rapa yeye akaja kufunga kazi kwa usiku huo, huku akiitroduce Single yake mpya.