Burudani
Dudubaya atangaza kuacha pombe
Katika kuonyesha wasanii kila kukicha wanafikiria mapya na kugundua makosa yao wamekuwa wakibadilika kila kukicha. Hivi juzi juzi msanii fulani alitangaza kuachana na kitu cha majani aka Khush… hivi sasa naye
msanii Godfrey Tumaini aka Dudubaya aka Mamba, ameandika katika mtandao wa Facebook kwamba ameagana kabisa na unywaji wa pombe. jambo hili nadhani linatia tumaini na huenda kuna wasanii mbalimbali, ambao wanajijua wakipata kidogo, basi wanakosa uwezo wa kustaamili na kuanzisha varangati, huenda na wao kwa sasa wakasema Basiiiiiiii… Ulevi ni Noma.