Burudani
Fally Ipupa kuachia albamu mpya mwezi Julai
Fally Ipupa ameahidi kuachia albamu yake mpya Julai 7 mwaka huu.
Kupitia mtandao wa Twitter, msanii huyo kutoka Congo DRC ametaja jina la albamu hiyo ni ‘Tokooos’.
“Albamu mpya #Tokooos July 7 ? – Inapatikana katika digital awali kuanzia Ijumaa,” ameandika kwenye mtandao huo.