Burudani

Fiesta 2010 kuanzia Mkoani Morogoro

Tamasha la Fiesta 2010 linakaribia kuanza,na kama ujuavyo tamasha hilo husheheni mambo kibao kwa wapenzi/washabiki wao.safari hii kwa mara ya kwanza tena linagonga hodi ndani ya mji kasoro bahari,Morogoro.Wakazi wa Morogoro Fiesta hiyo 2010 inawajia mkoani mwenu ikiwa na kauli mbiu yake JIPANGUSE Rrrrrrrhhhhhhaaaaa..! Huku Mdhamini mkuu wa tamasha hio ambalo hufanyika mara moja kwa mwaka ni kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Ltd.

Orodha ya wasaniii utakao Jipanguse nao ndio kama hao hapo juu,si hao tu na kuna wegineo kadhaa wa kadhaa akiwemo Mwana Fa,Amini na Linah kutoka THT.Kutakuwepo na michezo mbalimbali,Fiesta Jipanguse rrrhhhhhaaaaa 2010 itafanyika ndani ya uwanja wa Jamhuri,July 7 kwa kiingilio cha sh 2000 kwa kila mmoja.Kama vile haitoshi July 9 tamasaha hilo litahamia mjini Arusha na kufanyika ndani ya Matongee .

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents