Habari
Fundi wa MV. Nyerere apatikana akiwa hai
Mmoja wa Mainjinia wa Kivuko cha Mv.Nyerere kilichopata ajali ya kuzama ziwa Victoria, Alphonce Chelehani ameokolewa muda mfupi uliopita akiwa hai, mpaka sasa idadi ya miili iliyoopolewa ni 163.
Imeripotiwa zaidi ya watu 500 wakwama kwenda kutambua miili ya ndugu zao Ukara
Imeripotiwa Zaidi ya wananchi 500 wamekwama katika eneo la Bugolora baada ya kukosa usafiri wa kuelekea kisiwa cha Ukara kulikotokea ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere juzi Septemba 20, 2018. Wanachi hao wamekwama kutokana na usafiri kuwa wa shida kwani watu wengi sana wanaelekea eneo hilo wakiwemo viongozi wa Serikali.