Burudani
Harmonize afunguka “Labda hiyo ndio sababu ya kuniona mimi ni namba moja Tanzania” (Video)
Msanii wa muziki Harmonize amefunguka kuzungumzia maandalizi ya uzinduzi wa albamu yake Afro East ambayo inatarajiwa kuzinduliwa siku ya kesho katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Muimbaji amedai tukio hilo maalum litahudhuriwa na watu 500 licha ya wengi kutaka kushuhudia. Katika hatua nyingine rais huyo wa Konde Gang amezungumzia sababu ya wasanii wengi wa nje kusema yeye ni msanii namba moja nchini Tanzania.