Harusi ya Lionel Messi kufuru (Video+Picha)
Mchezaji wa timu ya taifa ya Argentina na klabu ya Barcelona, Lionel Messi amemuoa mpenzi wake wa muda mrefu, Antonela Roccuzzo hapo jana katika hoteli ya kifahari ya Rosario nchini Argentina.
Lionel Messi akiwa na mkewake, Antonela Roccuzzo
Messi mwenye umri wa miaka, 30 na mkewe Antonela Roccuzzo , 29 wamekuwa wapenzi tangu utotoni huku familia zao zikiwa majirani. Harusi hiyo ya mchezaji bora wa dunia ilikuwa na wageni waalikwa 260 pekee huku maelfu ya askari polisi wakitanda maeneo hayo ya harusi.
Lionel Messi akiwa na mkewake, Antonela Roccuzzo
Messi alikutana na Roccuzzo akiwa na umri wa miaka 13 kabla ya kuhamia Hispania.
Mama yake Messi Celia, baba yake Jorge na dada yake Maria wakifika kwenye harusi ya Messi
Miongoni mwa wageni waalikwa hapo jana siku ya Ijumaa nipamoja na Luis Suárez, Neymar, Gerard Piqué akiwa na mkewe Shakira, wageni wengi wali wasili na ndege binafsi, magazeti ya nchini Argentina yameandika kuwa hiyo ni arusi ya mwaka.
Xavi Hernandez, Cesc Fabregas na Carles Puyol wakiwasili na wakezao
Mchezaji wa Argentine Ezequiel Lavezzi akiwa na Latina katika red kapeti
Rosario Hotel City Center ikiwa imeandaliwa kwaajili ya shukhuli hiyo
Mchoraji, Lisandro Urteaga akichora picha ya Messi katika ukuta Rosario huku ndoa ikiwa inaendelea
Wananchi wakiwa nje ya hoteli ya Rosario wakitaka kushuhudia kinachoendelea
By Hamza fumo