Hili ndio gari lenye bei ghali zaidi duniani, gharama yake inazidi bajeti ya mwaka ya wizara ya habari
Kampuni ya kutengeneza magari ya nchini Ufaransa ya Bugatti, wiki iliyopita imezindua gari lake jipya la kwanza lenye gharama kubwa zaidi duniani kwa muda wote.
Gari hilo aina ya Bugatti La Voiture Noir ndio gari la gharama kubwa hadi sasa mwaka 2019, ambapo linauzwa kwa Dola Milioni $19 sawa na Tsh Bilioni 44 bila kodi.
Gari hilo ambalo tayari limeshanunuliwa na mteja mmoja kutoka Ujerumani, limetengenezwa maalum kwa ajili ya kusherehekea miaka 110 ya kampuni ya hiyo.
Gari la Bugatti La Voiture Noir limevunja rekodi ya kuwa gari lenye bei ghali zaidi duniani, rekodi hiyo awali ilikuwa inashikiliwa na gari aina ya Rolls-Royce Sweptail, lililokuwa linauzwa Dola Milioni $13 Sawa na takribani Bilioni 30 za Kitanzania.
Gari hilo ambalo tayari limeshanunuliwa na mtu mmoja kutoka Ujerumani, ambaye hakutaka jina lake litajwe, bado halijatajwa sifa zake ikiwemo spidi.
Tazama orodha ya magari yenye bei ghali zaidi duniani kabla ya toleo hili jipya kutangazwa.
Model | Price |
Rolls-Royce Sweptail | $13 million |
Mercedes-Benz Maybach Exelero | $8 million |
Koenigsegg CCXR Trevita | $4.8 million |
Lamborghini Veneno | $4.5 million |
W Motors Lykan Hypersport | $3.4 million |
Limited Edition Bugatti Veyron by Mansory Vivere | $3.4 million |
Ferrari Pininfarina Sergio | $3 million |
Bugatti Chiron | $2.9 million |
Laferrari FXX K | $2.7 million |
Aston Martin Valkyrie | $2.6 million |
Pagani Huayra BC | $2.6 million |
Mercedes-AMG One | $2.5 million |
Ferrari F60 America | $2.6 million |
Aston Martin Vulcan | $2.3 million |
Milan Red | $2.3 million |
McLaren Speedtail | $2.2 million |
Gharama za gari hilo yaani Tsh Bilioni 44 ni nyingi kuzidi Bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19 ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambayo ilikuwa ni Tsh Bilioni 33.