Hizi zinaweza kuwa ni picha bora na za ufundi Tanzania zilizopigwa mwaka jana
Fani ya upigaji picha inahitaji ubunifu kama zilivyo fani zingine kama uchoraji. Ndio maana fani hiyo hufundishwa chuoni ambapo wapiga picha pamoja na ujuzi wao binafsi huongezea maarifa zaidi katika kupiga picha zinazoongea.
Katika kutolea mfano wa ujuzi katika kupiga picha tumeamua kutumia mfano wa picha zinazopigwa na Pernille Bærendtsen (mwanamke) raia wa Denmark ambaye hufanya kazi kama mtaalam wa mawasiliano katika taasisi ya Dunia Duara.
Mpiga picha huyo amekuwa akihusika pia na kupiga picha za Zitto Kabwe na hizo ni miongoni mwa picha alizopiga mwaka jana zikiwemo zile za wasanii wa Kigoma Allstars.