Burudani
Jay Z atajwa ‘Hip-Hop Cash King’
Katika list iliyotolewa na kampuni inayohusika na uhasibu ya Forbes ya nchini Marekani, Rapper Jay Z ametajwa kama tajiri kuliko rapper yeyote duniani.
Rapper huyo ameonyesha kuwa kipato cha kiasi cha dola millioni 63 kati ya mwaka 2009 na mwaka huu wa 2010,kutoka katika biashara mbalimbali na pia ile kutokana na Muziki wake.
Rapper huyo amefuatiwa na Sean P ‘Diddy’ Combs akiwa na kipato cha dola millioni 30, na Akon akimfuatia akiwa na Kipato ch dola milioni 21.
Jay Z anasadikika kulipa mpaka kiasi cha dola milioni 22 kama kodi kwa serikali ya Marekani.