Michezo
Joe Hart kujiunga na Torino ya Italia kwa mkopo
Golikipa wa timu ya taifa ya England Joe Hart ambae kwasasa hana namba katika kikosi cha kwanza cha Man City, chini ya kocha mpya Pep Guardiola.
Hart ambaye hajaanza katika michezo mitatu iliyopita ya ligi kuu ya England, nafasi yake imekuwa ikichukuliwa na na kipa mkongwe Willy Caballero.
Taarifa zinasema kipa huyo anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya leo hii ili kujiunga na timu ya Torino ya nchi italia,kwa mkopo.
Man City tayari wamemsajili golikipa Claudio Bravo toka Barca kwa mkataba wa miaka minne.