Michezo
Joshua amtamani Fury kabla ya kukutana na Klitschko
Bondia wa uzito wa juu duniani, Anthony Joshua anahitaji pambano dhidi ya Tyson Fury.
Bondia wa uzito wa juu duniani, Anthony Joshua
Joshua mwenye umri wa miaka 27, ameomba pambano hilo huku akimsubiria Wladimir Klitschko kama atakubali kucheza mchezo wao wa marudiano wa ubingwa wa uzito wa juu mwezi Novemba mwaka huu.
“Ninasikiliza kile watu wanacho hitaji. Tyson amezungumza sana ujinga na kusema anahitaji kupigana na mimi,” ameliambia shirikisho la habari la Sky Sports News HQ
“Sasa ninamuambia mwenyewe nahitaji vilevile kupambana na wewe tuwache watu wapate kile wanachotaka kutoka kwetu,” ameongeza.
Bondia asiyepigika ,Tyson Fury
BY HAMZA FUMO