KARIBU KWENYE FUNGUKA NA BONGO5
Ndugu wapenzi na wadau wa muziki, filamu na mambo yote yanayohusiana na sanaa hapa Tanzania, napenda kuwataarifa kwamba kutakuwa na sehemu maalum ambayo itakuwaweka huru kuongea na kujadilia jambo ambalo tutalitambulisha kwenu.
Wapenzi wa Bongo5, sisi tutakuwa tunawaleta picha za wasanii wawili au kundi la wasanii na kujadili kuhusu kitu wanachogombea, maelezo ya kuwa nani zaidi, na mengine ambayo kwa mujibu wa maelezo ndivyo mdau atakavyochangia.
Tutaruhusu kutoa amaoni, ushauri, sifa, kokusoa, kuonya na hata kufundisha ilimradi kuzingatia maadili ya mtanzania na kutunza heshima ya kila mmoja, kwani lengo letu ni kukuza na kusahihishana juu ya jambo fulani.
Karibuni sana katika Page ya FUNGUKA NA BONGO5, na tunahitaji ufunguke kwelikweli ili kila mmoja ajue nini unakichangia, hii itakuwa kila jumamosi, kwaajili ya kuchangamshana na buludishana na hata kuonja kicheko kwa muda huo. By MO ONE’S