Burudani

Kava ya Money Mondays ya Vanessa Mdee yawekwa wazi

Dalili ya mvua ni mawingu. Hatimaye Vanessa Mdee ameachia kava la albamu yake mpya aliyoipa jina la ‘Money Mondays’ ambayo bado haijatoka.

Vee Money ameonyesha kava hilo kupitia mtandao wake wa Instagram na kuthibitisha hiyo ndio yenyewe kwa kuandika, “This is the official album cover #MoneyMondaysTheAlbum πŸΎπŸ™ŒπŸ½πŸ™πŸΎπŸ’«πŸ’«β‰οΈβ—οΈπŸŽβ‰οΈβ‰οΈπŸ’œπŸ‘©β€πŸŽ€ πŸ“Έ.”

Wakati akiongea na Bongo5 Jumanne hii, msanii huyo alisema albamu yake hiyo mpya itakuwa na nyimbo 18.

Albamu hiyo itatoka kabla ya mwaka huu kumalizika na miongoni mwa wasanii ambao watasikika kwenye albamu hiyo ni Cassper Nyovest wa Afrika Kusini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents