Burudani
Kava ya Money Mondays ya Vanessa Mdee yawekwa wazi
Dalili ya mvua ni mawingu. Hatimaye Vanessa Mdee ameachia kava la albamu yake mpya aliyoipa jina la ‘Money Mondays’ ambayo bado haijatoka.
Vee Money ameonyesha kava hilo kupitia mtandao wake wa Instagram na kuthibitisha hiyo ndio yenyewe kwa kuandika, “This is the official album cover #MoneyMondaysTheAlbum πΎππ½ππΎπ«π«βοΈβοΈπβοΈβοΈππ©βπ€ πΈ.”
Wakati akiongea na Bongo5 Jumanne hii, msanii huyo alisema albamu yake hiyo mpya itakuwa na nyimbo 18.
Albamu hiyo itatoka kabla ya mwaka huu kumalizika na miongoni mwa wasanii ambao watasikika kwenye albamu hiyo ni Cassper Nyovest wa Afrika Kusini.