Kilimanjaro si mchezo
Mastaa waliokuja nchini kupanda Mlima Kilimanjaro kwa ajili ya hisani wamekubali kwamba upandaji wa Mlima huo uliochukua siku 6 na maili 50 haukuwa lelemama na ilibidi kuongeza uvumilivu wa ziada kufanikisha zoezi hilo lililotazamwa na karibu dunia nzima likiwa na lengo la kusisitiza matumizi ya maji safi kwa nchi zinazoendelea. Kuwepo kwa gharika za mabarafu kulizidisha ugumu na kupunguza spidi ya upandaji
Jessica Biel kwenye harakati za kupanda Mlima
Kituo cha burudani cha MTV kitarusha makala ya dakika 90 ya tukio hilo Machi 14 kuanzia saa 9 usiku. Miongoni mwa mastaa hao ni Lupe Fiasco, Jessica Biel na Kenna