Habari
Kocha wa timu ya taifa, taifa stars aagwa rasmi
Aliyekuwa kocha Mkuu wa Taifa Stars, Marcio Maximo, ameagwa rasmi usiku wa kuamkia leo katika hafla fupi iliyoandaliwa na TFF Msasani jirani na shule ya Feza jijini Dar . Katika hafla hiyo, pamoja na mambo mengine, Kocha Maximo alipewa zawadi mbalimbali ikiwemo ya kinyago alichopewa na Mwenyekiti Mtendaji wa kiwanda cha Serengeti, Jaji Mark Bomani.
Ni dhahiri kwamba kocha huyo atakumbukwa kwa kazi yake aliyoifanyia Tanzania japokuwa bado kuna wadau wa soka ambao wanasema hakufaya kitu ila tunaojua kusema asante tunasema Maximo amefanya kitu kikubwa katika soka letu lililokuwa la kichwa cha Mwendawazimu enzi hizo, na anastahili kupongezwa mpaka hapa alipotufikisha manake kuna methali inayosema “Mnyonge Mnyongeni lakini haki yake mpeni”