Michezo
Lewis Hamilton achukua taji la Japan GP
Dereva wa magari yaendayo kasi Lewis Hamilton kutoka timu ya Mercedes ameshinda michuano ya Suzuki na kutwaa taji la 41 katika mchezo huo.
Lewis Hamilton akiwa ameshikilia taji la Japan GP na Nico Rosberg (kushoto) akishika nafasi ya pili huku Sebastian Vettel (kulia) akishika nafasi ya tatu
Hamilton alishinda taji hilo na kumfikia mkongwe wa michuano ya Fomula 1 Mbrazili Ayrton Senna. Hamilton alimzidi kwa alama 48 dereva mwenzake wa timu ya Mercedes, Nico Rosberg, katika mbio za michuano hiyo ya Grand prix.
Kumesalia mbio tano Hamilton, akiwa na alama 48 zaidi ya Rosberg, huku akionekana na uwezo wa kushinda taji lingine la tatu la Fomula 1.