Lionel Messi ashinda tuzo nyingine, orodha kamili ipo hapa
Superstar wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2015 (Globe Soccer Awards) inayotolewa kila mwaka.
Lionel Messi akipokea tuzo yake ya heshima ya mchezaji bora wa mwaka kutoka Globe Soccer, Dubai
Globe Soccer Awards 2015 zilizotolewa huko Dubai na ni tuzo maalum kwa ajili ya wanasoka, viongozi bora wa klabu, wakala bora, kocha bora.
Legend wa Italia Andrea Pirlo alishinda tuzo ya heshima baada ya Globe Soccer kutambua mchango wake kwenye soka
Ni tuzo ambazo zinatolewa kwa uandaaji au ushirikiano wa chama cha mawakala wa wachezaji soka barani Ulaya EFAA (European Association of Player’s Agents) na umoja wa vilabu vya soka barani Ulaya ECA (European Club Association).
Frank Lampard alishinda tuzo ya heshima baada ya Globe Soccer kutambua mchango wake kwenye soka
Jorge Mendez alishinda tuzo ya wakala bora wa mwaka
Kocha wa Ubelgiji Marc Wilmots (kushoto) akipokea tuzo ya kocha bora wa mwaka
Hii ndio list ya washindi wa tuzo hizo kwa mwaka 2015.
Lionel Messi (Mchezaji bora wa mwaka)
FC Barcelona (Klabu bora kwa mwaka)
Jorges Mendes (Wakala bora wa mwaka)
Marc Wilmots (Kocha bora wa mwaka)
S.L BENFICA (Acadeny bora ya mwaka)
Ravshan Irmatov (Refa bora wa mwaka)
Josep Maria Bartomeu (Rais bora wa klabu)
Andrea Pirlo (Life time Archivement)
Frank Lampard (Life time Archivement)