Lupe Fiasco ndani ya Bongo
Msanii wa Marekani, Lupe Fiasco, yupo nchini tangu Januari 11 akipanda mlima Kilimanjaro kwa hisani kwenye kampeni ya kusisistiza matumizi ya maji safi katika nchin zinazoendelea. Miongoni mwa watu maarufu walioambatana na msanii huyo, ni mwigizaji wa Marekani Jessica Biel na mwanamuziki Kenna mwenye asili ya Ethiopia. Upandaji wa mlima huo utachukua siku saba na baada ya hapo jamaa atarudi kwao kuendele kula bata. Shughuli hiyo imedhaminiwa na kituo cha burudani cha MTV