Burudani
Madee amtaja ni mchezaji yupi mkali kati ya Ronaldo na Messi
Licha ya kufanya muziki, muimbaji wa ‘Vuvula’ Madee ni shabiki mzuri wa soka.
Hivi karibuni Madee alikuwa akiongea na kipindi cha Sports Xtra cha Clouds FM na aliulizwa na Shaffih Dauda kuwa yeye ni shabiki wa mchezaji gani kati ya Cristiano Ronaldo na Lionel Messi na nani mchezaji mkali kati yao.
“Messi amecheza Barcelona kwa muda mrefu na amekuwa bora kwa pale na tunakubali,” alijibu.
“Lakini mchezaji mkali lazima aweze kufanya vizuri akiwa na wachezaji tofauti kwenye mazingira tofauti na timu tofauti kwa mawazo yangu. Mimi nimemuona Ronaldo akiwa kwenye level ya juu akiwa Manchester na Real Madrid. Lakini Messi sijui kama akiwa Manchester atakuwa na kiwango kile kile? Ssasa mimi namkubali Ronaldo japokua Messi na yeye mkali.”